Wiki
ya 52 ya mwaka 2015 imekuwa ya matukio mbalimbali kwa wanachama wa Jumuiya ya
Marafiki wa Kinondoni, katika wiki hii wanachama wawili wa Jumuiya
wamesherehekea siku zao za kuzaliwa. Wanachama hao Bi. Remina Omary na Bi. Anna
Mwengele wote wamezaliwa siku moja, yaani tarehe 22 mwezi Disemba.
![]() |
| Add caption |
Kama
ilivyo ada, Wanajumuiya hawakukosa katika kuwapongeza wanachama wenzao hao katika
siku hiyo. Tirika na picha mbalimbali za tukio hilo hapa chini.
![]() |
| Remina Omari (katikati) akiwa pamoja na Abdul Kazembe (kushoto) na Mkala Fundikira (kulia) |
![]() |
| Keki nazo zilikuwepo |
![]() |
| Selfie ilihusika pia |
Tukio lingine
ni ajali aliyopata mwenyekiti wa Jumuiya ndugu Yahya Poli iliyosababishwa na
bodaboda. Wanajumuiya wamemtumia salamu za pole Mwenyekiti wao na
kumuombea apone haraka ili aendelee na majumukumu yake ya kuijenga Jumuiya.
![]() |
| Sehemu ya jeraha alilopata Mwenyekiti baada ya matibabu |
Mwanajumuiya, Esther
Shayo naye wiki hii alizawadiwa tuzo ya mfanyakazi bora wa mwaka 2015 kwa
wafanyakazi wa kampuni ya Porter Noveli. Wanajumuiya wanampongeza dada Esther
kwa tuzo hiyo na wamemkumbusha kuwa tuzo hiyo ni changamoto y kuongeza bidii
zaidi kazini. Vilevile wanajumuiya walishauri uongozi wa Jumuiya kuangalia
uwezekano wa kuwa tuzo mbalimbali za mwaka kwa wanachama wake na ikiwezekana
iwe ni kuanzia mwaka 2016.
![]() |
| Tuzo ya mfanyakazi Bora - 2015 |
![]() |
| Makamu Mwenyekiti MKala Fundikira (mbele) akiwa na nfanyakazi bora Esther Shayo |
Katika kumalizia
wiki hii pia Wanajumuiya watasherehekea sikukuu za kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
(S.A.W) ambayo inasherehekewa tarehe 12 Rabi
Al-Awaal 1437 A.H. sawa na tarehe 24 Disemba, 2015
Vilevile sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo ambayo husherehekewa tarehe 25
Disemba ya kila mwaka.
Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni inawatakia wanachama
wake na watu wote duniani heri ya sikukuu za Maulid na Krismasi na pia inawaasa
kuzisherehekea siku hizo kwa kutenda matendo ya huruma nay a mpendezayo Mungu.









No comments:
Post a Comment