Thursday 31 December 2015

SALAAM ZA MWAKA MPYA 2016 TOKA JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI





JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI

SALAM ZA MWAKA MPYA 2016

Wanajumuiya,
Ni matumaini ya kila mmoja wetu kwamba mwaka huu 2015 unaisha ukiwa  na changamoto na mafanikio yake. Kwa ujumla, kama Jumuiya mwaka 2015 umekuwa ni mwaka wa mafanikio kwetu tangu tulipoona hitaji la kuwa Jumuiya na tulipoanza utekelezaji wake kwa mbinu na njia mbalimbali. Sote tunakumbuka jitihada tulizofanya katika kuhakikisha Jumuiya yetu inasimama imara na wote tumejitolea kwa hali na mali katika kufanikisha jambo hilo.

Wanajumuiya,
Ni takriban miezi mine (4) tu tangu tuirasimishe Jumuiya yetu kwa kuandaa Katiba na baadaye kufanya uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya ambao wanatarajiwa kuhudumia Jumuiya kwa kipindi cha miaka mitati (3) kuanzia mwezi Septemba, 2015 mpaka Septemba, 2018. Hadi kufikia tarehe 31 Disemba, 2015, Jumuiya ina jumla ya wanachama 41. Wanachama hawa wote kwa pamoja wana lengo la kuifanya Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni kuwa ni Jumuiya yenye kuwaunganisha pamoja wakati wote na kuwaletea manufaa. Kimsingi Jumuiy, kama taasisi au mkusnyiko mwingine wowote, ina malengo mbalimbali ambayo ni ya muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu kama ifuatavyo:  -
1.   Malengo ya muda mfupi ((Oktoba 2015 – Machi, 2016)

1.1.      Kusajili jumuiya katika mamlaka za nchi  ili kuifanya iwe rasmi na itambulike kisheria,

1.2.      Kufungua akaunti ya benki,

1.3.      Kupanga ofisi ya Jumuiya,

1.4.      Kuongeza idadi ya wanachama,

1.5.      Kuendelea kukusanya michango na ada mbalimbali toka kwa wanachama ili kukuza mifuko mbalimbali ya Jumuiya.


2.   Malengo ya muda wa kati (Machi 2016 – Machi, 2018)

2.1.      Kubaini fursa mbalimbali za kiuchumi na kimaendeleo kwa Jumuiya,

2.2.      Kuwezesha upatikanaji wa huduma za bima ya afya kwa wanachama wote,

2.3.      Kuanzisha na kuingia ubia wa kibiashara kati ya Jumuiya na Wanajumuiya,

2.4.      Kuanzisha chama cha akiba na mikopo (SACCOS) kwa wanachama na jamii kwa ujumla,

2.5.      Kuongeza idadi ya wanachama,

2.6.      Kuendelea kukusanya michango, ada na tozo mbalimbali toka kwa Wanajumuiya

3.   Malengo ya muda mrefu (2015 na kuendelea)

3.1.      Kuwekeza katika miradi ya ardhi, kilimo na ufugaji,

3.2.      Kuchangia gharama za elimu kwa wanajumuiya wenyewe na watoto/wategemezi wao,

3.3.      Kumiliki eneo (estate) la Jumuiya litakalokuwa na huduma zote za kijamii kama vile, nyumba za makazi za wanajumuiya na familia zao, shule, hospitali, soko, maduka madogo na makubwa, viwanja vya michezo, n.k.

3.4.      Kuingia ubia na kununua hisa kwenye makampuni mbalimbali,

3.5.      Kuanzisha viwanda vidogo vidogo na vikubwa,

3.6.      Kufungua kampuni zitakazojihusisha na biashara mbalimbali,

3.7.      Kuongeza idadi ya wanachama,

3.8.      Kuendelea kukusanya michango, ada na tozo mbalimbali toka kwa Wanajumuiya. 

Wanajumuiya,
Tukiyasoma na kuyatafakari haya malengo yote, tunajifunza kwamba hakuna linaloshindikana iwapo wote tutakuwa na lengo la kutumia vyema fursa vipaji na nafasi tulizonazo katika kuyatimiza yote. Lakini pia, ni ukweli kwamba bila ya nguvu kubwa ya kiuchumi inaweza kutugharimu muda mrefu kufikia angalau robo ya malengo hayo. Yatakapotimia itakuwa ni faida kubwa kwetu sote na vizazi vyetu!

Wanajumuiya,
Mwaka 2016 ni mwaka wetu wa kuthibitisha kuwa sisi ni Jumuiya ya kutolewa mfano kwa masuala yote yanayohusu Jumuiya kama yetu au zinazofanana na Jumuiya yetu. Mtaji mkubwa kabisa tulionao ni huu umoja wetu, kujitoa na kujitolea kwetu na zaidi upendo na ushirikiano wetu. Kila mmoja akitimiza wajibu wake ipasavyo, hakuna litkalotushinda huko mbele!


Wanajumuiya,
Kwa niaba ya viongozi wote wa Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni, nawatakia heri, baraka, afya njema na mafanikio tele katika mwaka 2016 na miaka mingine yote ijayo.


Yahya Poli,
Mwenyekiti – jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni,

Wasiliana nasi: - 
Twitter: @rafikinondoni
Instagram: rafiki_kinondoni


Thursday 24 December 2015

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA WIKI YA 52 YA MWAKA 2015 KWA JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI

Wiki ya 52 ya mwaka 2015 imekuwa ya matukio mbalimbali kwa wanachama wa Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni, katika wiki hii wanachama wawili wa Jumuiya wamesherehekea siku zao za kuzaliwa. Wanachama hao Bi. Remina Omary na Bi. Anna Mwengele wote wamezaliwa siku moja, yaani tarehe 22 mwezi Disemba.

Add caption
Kama ilivyo ada, Wanajumuiya hawakukosa katika kuwapongeza wanachama wenzao hao katika siku hiyo. Tirika na picha mbalimbali za tukio hilo hapa chini.
Remina Omari (katikati) akiwa pamoja na Abdul Kazembe (kushoto) na Mkala Fundikira (kulia)


Keki nazo zilikuwepo
Selfie ilihusika pia
 Tukio lingine ni ajali aliyopata mwenyekiti wa Jumuiya ndugu Yahya Poli iliyosababishwa na bodaboda. Wanajumuiya wamemtumia salamu za pole Mwenyekiti wao na kumuombea apone haraka ili aendelee na majumukumu yake ya kuijenga Jumuiya.
Sehemu ya jeraha alilopata Mwenyekiti baada ya matibabu
Mwanajumuiya, Esther Shayo naye wiki hii alizawadiwa tuzo ya mfanyakazi bora wa mwaka 2015 kwa wafanyakazi wa kampuni ya Porter Noveli. Wanajumuiya wanampongeza dada Esther kwa tuzo hiyo na wamemkumbusha kuwa tuzo hiyo ni changamoto y kuongeza bidii zaidi kazini. Vilevile wanajumuiya walishauri uongozi wa Jumuiya kuangalia uwezekano wa kuwa tuzo mbalimbali za mwaka kwa wanachama wake na ikiwezekana iwe ni kuanzia mwaka 2016.


Tuzo ya mfanyakazi Bora - 2015

Makamu Mwenyekiti MKala Fundikira (mbele) akiwa na nfanyakazi bora Esther Shayo
Katika kumalizia wiki hii pia Wanajumuiya watasherehekea sikukuu za kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) ambayo inasherehekewa tarehe 12 Rabi Al-Awaal 1437 A.H. sawa na tarehe 24 Disemba, 2015



Vilevile sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo ambayo husherehekewa tarehe 25 Disemba ya kila mwaka.


Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni inawatakia wanachama wake na watu wote duniani heri ya sikukuu za Maulid na Krismasi na pia inawaasa kuzisherehekea siku hizo kwa kutenda matendo ya huruma nay a mpendezayo Mungu. 

Wednesday 23 December 2015

ANNA MWENGELE: KARIBU KATIKA JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI

Jumuiya ya Marafiki wa Kiondoni inazidi kupata wanachama wapya. Tarehe 19 Disemba, 2015 Mwanajumuiya mpya alijiunga rasmi katika Jumuiya hiyo, BI. Anna Mwengele (pichani chini) akizungumzia namna alivyoifahamu Jumuiya alieleza kuwa mwanzoni alidhani ni “group” tu la kuchati mtandaoni, lakini baada ya kukutana na Wanajumuiya na kupata taarifa zote kuhusu Jumuiya, hakutaka kusubiri hata kidogo na badala yake alifuata taratibu zote za kujiunga na Jumuiya na amekuwa Mwanachama wa 41.

Anna Mwengele - Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni
Akimkaribisha rasmi katika Jumuiya, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Marfiki wa Kinondoni, ndugu Ivan Minja alimuasa bi Anna Mwengele kushiriki kikamilifu katika masuala yote ya Jumuiya na pia kutoa maoni, mawazo pamoja na kutumia kipaji chake pamoja na fursa mbalimbali katika kuyafikia malengo ya Jumuiya.

Akizungumza baada ya kukaribishwa rasmi kwenye Jumuiya, Bi. Anna alieleza furaha yake kuwa sehemu ya Jumuiya muhimu kwa maendeleo ya Wanakinondoni na ameridhishwa na namna Wanajumuiya wanavyojitolea katika masuala mbalimbali ya kijamii. Vilevile amewasisitiza Wanajumuiya wote uendeleza upendo na ushirikiano alioukuta na hiyo ndio iwe falsafa ya wote katika kuyafikia malengo ya Jumuiya. 

PUMZIKA KWA AMANI (R.I.P) MLAWILA "LAWI" MGALULA FUNDIKIRA

Usiku wa tarehe 18 Disemba 2015, Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni ilipata msiba mkubwa wa kijana Mlawila "Lawi" Mgalula Fundikira aqmbaye ni mtoto wa mwanajumuiya Mgalula Fundikira ambaye alikuwa katika uangalizi maalum wa kitabibu (ICU) kwa takriban juma moja katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kutokana na majeraha ya ajali. Makamu mwenyekiti wa Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni ndugu Mkala Fundikira, ambaye pia ni baba mdogo wa marehemu Lawi alitoa taarifa ya msiba huo kwa masikitiko makubwa ambapo mipango ya mazishi ilifanyika nyumbani kwa baba wa marehemu na mazishi yalifanyika katika makaburi ya Kisutu Dar es Salaam siku ya jumapili tarehe 19 Disemba, 2015.
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya: Mkala Fundikira (kulia) akiwa pamoja na Wanajumuiya 

Baada ya kukamilisha shughuli za msiba, Mwanajumuiya Mgalula Fundikira alitoa salamu za shukrani wa wote walioshiriki msiba wa kijana wake aliandika haya: - 
"To my dear family and friends, My son Mlawila "Lawi" has finally been laid to rest and i am coming to accent however slowly and painfully that he is now in a better place, No words can ever express the way you all have made me feel during this most trying and difficult period in my life, I convey my utmost sincere gratitudes and appreciation for all the love, support and solidarity you have shared with my us and still do, On behalf of Mama Lawi, Nyanzala, Oliver and the rest of the Fundikira family, I can simply say Thank you all, Please keep on staying as amazing as you all have been, Much love and respect to all of you, Rest in Peace my son."

Pumzika kwa Amani (R.I.P) Mlawila "Lawi" Mgalula Fundikira.

Sunday 13 December 2015

IJUE KATIBA YA JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI

Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni ni umoja na rasmi na unaongozwa na katiba inayojulikana kama Katiba ya Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni (2015). Katiba hiyo yenye Ibara 8 itakuwa mwongozo wa msingi na itasomwa pamoja na Kanuni mbalimbali na nyaraka nyinginezo ili kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali. Mtiririko wa Ibara za Katiba ya Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni ni kama ufuatao: -

 IBARA YA KWANZA
JINA, ANUANI NA LUGHA RASMI
1.1. Jina la Jumuiya
1.2. Anuani
1.3. Lugha Rasmi

IBARA YA PILI
LENGO KUU NA MALENGO MAHUSUSI
1.1. Lengo Kuu
1.2. Malengo Mahususi

IBARA YA TATU
SIFA, UTARATIBU WA KUJIUNGA, HAKI, WAJIBU NA UKOMO
3.1. Sifa za Kuwa Mwanajumuiya
3.2. Utaratibu wa kujiunga na Jumuiya
3.3. Haki za Mwanajumuiya
3.4. Wajibu wa Mwanajumuiya
3.5. Ukomo wa Mwanajumuiya

IBARA YA NNE
SIFA ZA VIONGOZI NA MUUNDO WA UONGOZI
4.1. Sifa za Viongozi
4.2. Muundo wa Uongozi

IBARA YA TANO
VIKAO MAHUSUSI
5.1. Vikao Mahususi vya Jumuiya

IBARA YA SITA
MAPATO, UENDESHAJI WA AKAUNTI NA MATUMIZI
6.1. Mapato ya Jumuiya
6.2. Uendeshaji wa Akaunti ya Jumuiya
6.3. Matumizi ya Jumuiya

 IBARA YA SABA
MAREKEBISHO YA KATIBA, UTATUZI WA MIGOGORO NA KUVUNJWA KWA JUMUIYA 7.1. Marekebisho ya Katiba
7.2. Utatuzi wa Migogoro katika Jumuiya
7.3. Kuvunjwa kwa Jumuiya

IBARA YA NANE
KUTUMIKA KWA KATIBA
8.1. Marekebisho ya Katiba
Katiba hiyo inauzwa Tshs. 10,000/=

Kama una swali, maoni au jambo lolote kuhusu Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni, tuandikie barua pepe marafiki.kinondoni@gmail.com au tupigie simu  0656 974 983 (Katibu Mkuu).

JE, UNGEPENDA KUIJUA NA HATIMAYE KUJIUNGA NA JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI?

Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni inapenda kuwakaribisha watu wote wanaokidhi vigezo na masharti ya kujiunga na wangependa kuwa sehemu ya Jumuiya. Utaratibu wa kujiunga na jumuiya ni kama ufuatao: -

  1. Nunua fomu ya maombi ya uanachama  kwa kulipia Tsh. 10,000/= kwa kutuma kwenye namba hii 0676 330 338 (Ismail Kagambo) tigo-pesa, ada hii haitarudishwa (non-refundable),
  2. Baada ya kulipia tuma sms kwa namba hii 0712 831 052 ukitoa taarifa ya kufanya malipo husika,
  3. Katibu wa Jumuiya atakuelekeza utaratibu wa kuipata fomu yako ya maombiya uanachama pamoja na maelekezo mengine.
FOMU YA MAOMBI YA UANACHAMA WA JUMUIYA YA MARAFIKI WA KINONDONI.pdf by Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni

NB:
Katibu atakujulisha juu ya hatma ya maombi yako na kukupa maelekezo ya kina juu ya hatua zote zinazofuata ili kukamilisha utaratibu wa kujiunga na Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni iwapo maombi yako yatakubaliwa.

Kama una swali, maoni au jambo lolote kuhusu Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni, tuandikie barua pepe marafiki.kinondoni@gmail.com au tupigie simu  0656 974 983 (Katibu Mkuu).

    Wednesday 9 December 2015

    HERI YA SIKU YA KUZALIWA: DADA JULIANA KITUNDU ASHEREHEKEA SIKU YA KUZALIWA LEO TAREHE 9 DISEMBA, 2015

    Wakati Tanganyika ikisherehekea miaka 54 tangu kupata uhuru, Mwanachama na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya  wa Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni, dada Juliana Kitundu (pichani chini) anasherehekea siku ya kuzaliwa. 

    JULIANA KITUNDU

    Jumuiya ya Marafiki wa Kinondoni inamtakia mwanachama wake heri ya siku ya kuzaliwa na mwenyezi ampe maisha marefu yenye afya na mafanikio tele! 

    Dada Juliana akiwa makini kujdili jambo na Adam Bush





    Dada Juliana (mwenye blausi ya njano)akiwa katika picha ya pamoja na Wanajumuya wenzake
    Keki itakatwa jioni ya leo na itataarifiwa ni wapi na muda gani!